Zaburi 29:1-11

Swahili Union Version (SUV)

1Mpeni Bwana, enyi wana wa Mungu, Mpeni Bwana utukufu na nguvu;

2Mpeni Bwana utukufu wa jina lake; Mwabuduni Bwana kwa uzuri wa utakatifu.

3Sauti ya Bwana i juu ya maji; Mungu wa utukufu alipiga radi; Bwana yu juu ya maji mengi.

4Sauti ya Bwana ina nguvu; Sauti ya Bwana ina adhama;

5Sauti ya Bwana yaivunja mierezi; Naam, Bwana aivunjavunja mierezi ya Lebanoni;

6Airusharusha kama ndama wa ng'ombe; Lebanoni na Sirioni kama mwananyati.

7Sauti ya Bwana yaipasua miali ya moto;

8Sauti ya Bwana yalitetemesha jangwa; Bwana alitetemesha jangwa la Kadeshi.

9Sauti ya Bwana yawazalisha ayala, Na kuifichua misitu; Na ndani ya hekalu lake Wanasema wote, Utukufu.

10Bwana aliketi juu ya Gharika; Naam, Bwana ameketi hali ya mfalme milele.

11Bwana atawapa watu wake nguvu; Bwana atawabariki watu wake kwa amani.